Search This Blog

Tuesday, July 20, 2010

Underage Marriages

Premature Marriages in ‘SukumaLand” are disastrous, Should be discouraged

Column

Snap-Shots at Life

With Angel Navuri


I chanced to visit what is loosely known as Sukumaland (Mwanza/Shinganga regions recently sponsored by Women Dignity, and was acutely saddened by the discovery that negative cultural believes hold sway.

One of these is bride price, whereby some parents treat their daughters as commodities for sale to marital sitors, thereby blocking their prospects for a reasonable level of education.

In addition to that, girls are married off at a relatively tender age and their health is thus affected, on account of premature motherhood, In Bariadi, I saw under 18 girls who had been forced into marriage (put crudely and accurately, sold)by in exchange for dowry in form of cattle.

I was reliable told that a wife obliged to give to a given number of children according to the number of cows her parents received as dowry. this is a case of gross inhumanity, compounded by the fact that, in the first place, a girl is not given a chance to choose a man she fancies, but has to contend with someone imposed on her. another choice she isn’t afforded the opportunity to make is to put off any talk and propositions on marriage until she advances herself reasonable in education and vocational fields.

The Bariadi district hospital clinical officer, James Mranga, told me that the problem of forced marriages for girls aged below 18 was high, and that the victims had to give in because disobeying parents was taboo.

Regina Maluga, a mother who had brought her child to the hospital for treatment, said her father was given a bride of 10 cows for which she had to give birth to five children, which are two cows per child.

Maluga noted that if she didn’t give birth to five children, for the 10 cows paid top her parents as bride price, it would bring shame to her family, she lamented” the practice affects us because even if we need to have fewer children it is impossible as we have to pay back by bearing children to a specified chidren –cattle ration” The clinical officer said men needed family planning education more than women because they seemed to be more obstacle towards the implementation of family planning programme.he noted that even if the women wanted to start family planning they couldn’t because men needed more children.

I think more education is needed for the community and village leaders because this is denying the girls the right to education, its high time negative cultural beliefs were fought.

In chit-chats with a couple of women ,it transpired that if they opted for family planning, they have to use depo injection for family planning instead of pills because their husbands could find out.

For example the clinical Officer said that from January to May this year, only 30 women had undergone intra-uterine contraceptive device(IUCD),which was different in Karagwe district,Kagera Region ,where in one month only about 700 women decided to go for birth control. He also said they had been conducting public awareness programes on the importance of having a manageable number of children, but the fertility rate had remained high.

The parents have understood that early marriages have disadvantages like responsibility has to be shouldered at a very young age. One has to take on household responsibilities, child rearing responsibity, etc.

There is no adult to guide or help out missing out on the fun of teenage life and being young, the drudgeries of married life can overwhelm you. they deprive you and of your youth, often ,the young couple may not be able to pursuer higher education as they have to take on the responsibilities of family budget, and work opportunities of family budget, and work opportunities are limited for the youngsters.

Since their education levels are low they cannot get highly paid jobs, bringing up children care may be limited and parental guidance is also no there. they may not be able to provide the appropriate care for their children.

And Marrying early may seem very romantic and convenient, but it has its problems, couples need to get to know each other better and this takes time rushing into a marriage, which may not last long, does not appear the right thing to do ,in some countries ,where child marriage is prevalent ,efforts are on by respective governments to dissuade the practice .it is high time the Sukuma community changed for the better.



Angel Navuri is a journalist, The Guardian

Email.angelnavuri@yahoo.com

Wednesday, July 14, 2010

Story za Handeni

Burhani Yakub,Handeni.

ALIYEWAHI kuwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni,Luteni Mstaafu Winfred
Ligubi,amekumbukwa na wanawake wa kwa kitendo chake alichofanya
kumpiga makofi mwanaume aliyemkuta akitembea kwa maringo huku mkewe
mjamzito akiwa amebeba mzigo wa kuni na mtoto mgongoni.

Pongezi hizo walizitoa juzi walipokuwa wakizungumza na waandishi wa
habari waliokuwa Wilayani hapa kujifunza juu ya unyanyasaji,unyanyapaa
na ukatili wa kijinsia na masuala ya ukimwi yanayoendeshwa na Chama
cha waandishi wa habari za ukimwi (Ajat)

Wanawake hao wa kata ya Chanika,Wilayani hapa wamesema kuwa alipokuwa
Mkuu wa Wilaya moja Mkoani Tanga, Ligubi aliyekuwa katika safari
zake vijijini alimkuta mwanaume akitoka shambani akiwa amebeba
radio,lakini mkewe mjamzito alikuwa na mzigo wa kuni kichwani,mgongoni
kambeba mtoto na mikononi kashika majembe mawili.

Amina Mbughuni (44) mkazi wa mtaa wa Bomani Wilayani hapa,alisema Mkuu
huyo wa Wilaya anastahili pongezi za pekee kwa kitendo chake cha
kumuonea huruma mwanamke mwenzetu kufanyiwa ukatili wa kijinsia.

“Haya mambo yanafanyika sana hasa vijijini,na sisi huku tunaona ni
kitu cha kawaida tu,wanaume wanaona wao ni watu wa kustarehe na sisi
wa kumenyeka na kazi nyingi”alisema Amina.

Alisema mfumo dume umekithiri katika vijiji vya Wilaya ya Handeni na
kwamba wanawake hawana maamuzi hata katika kupanga mambo ya uzazi wa
mpango na ndiyo maana maambukizi ya ukimwi yamekuwa yakishamiri.

Mbuguni ambaye ni mjasiliamali alwaomba viongozi wengine kuiga m fano
wa Ligubi kwani watasaidia kuleta mabadiliko katika suala zima la
unyanyasaji wa kijinsia.

Wanawake hao walisema ili kuleta mabadiliko Serikali inapaswa
kuwasomesha maafisa maendeleo ya jamii wengi na kuwasamabaza vijiji
ili waweze kutoa msaada wa elimu ikiwamo kuwawezesha wanawake kutambua
haki zao za msingi.



Burhani Yakub,Handeni.

WILAYA ya Handeni inakadiriwa kuwa na zaidi ya watoto 6800 yatima
wakiwamo wanaoishi katika mazingira hatarishi pamoja na walea ambao
wazazi wao wamekufa kwa ugonjwa wa ukimwi.

Mratibu wa mpango shirikishi wa kudhibiti ukimwi Wilaya ya
Handeni,Thomas Mzinga, alitoa taarifa hiyo juzi wakati akizungumza na
waandishi wa habari waliokuwa Wilayani hapa kujifunza juu ya
unyanyasaji,unyanyapaa na ukatili wa kijinsia na masuala ya ukimwi
yanayoendeshwa na Chama cha waandishi wa habari za ukimwi (Ajat)

Alisema idadi hiyo ya watoto yatima inatokana na kuendelea kuongezeka
kwao kadiri siku zinavyozidi kusonga mbele hivyo yamefanyika makadirio
ya sensa iliyofanyika mwaka 2008 chini ya usimamizi wa Wizara ya Afya
na Mustawi wa jamii ambapo walikuwa 5200.

“Idadi ya watoto yatima Wilayani hapa imekuwa ikiongezeka kila kukicha
licha ya kuwa takwimu zinaonyesha kuwa maambukizi ya ukimwi yameanza
kupungua”alisema Mzinga.

Alisema kitaalamu ni kuwa licha ya kwamba maambukizi yameanza kupungua
lakini idadi ya wazazi wanaoendelea kufa ni wale wanaoishi na virusi
vya ukimwi ambavyo waliambukizwa miaka ya nyuma.

Mratibu huyo alisema katika kukabiliana na tatizo la watoto yatima na
wanaoishi katika mazingira magumu,Serikali imejikita katika
kuhakikisha wanapata elimu ambapo imekuwa ikiwalipia ada na
kuwanunulia vifaa vya shule.

Alisema katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2009/2010 Halmashauri ya
Wilaya ya Handeni ilipangiwa kupewa kiasi cha sh 57 milioni kwa ajili
ya shuhguli za kupambana na ukimwi ambapo katika robo ya kwanza
ziliwasilishwa sh 32 milioni.

Kwa mujibu wa maelezo ya maratibu huyo ni kuwa sh 32 milioni
zilizowasilishwa zilitumika kwa ajili ya kulipia ada na kuwanunulia
wanafunzi yatima waliopo katika shule mbalimbali za msingi na
sekondari.

MWISHO

Monday, July 12, 2010

STIGMA

UNYANYAPAA UNATUUA MAPEMA WAVIU.

N Hassan Simba, Lindi.

Julai 12, 2010. KUWAPO kwa tabia ya unyanyapaa miongoni mwa jamii dhidi ya watu wanaoishi na virusi vya ukimwi mkoani Lindi, kumeelezwa kuwa kunachangia kuwakwaza kiuchumi na kuzorotesha afya zao na kusababisha wengi wao kupoteza maisha mapema richa ya kuanza kutumia dawa za kupunguza makali ya ugonjwa huo ARVs.

Hayo yamebinishwa juzi na watu wanaoishi na virus vya ukimwi mkoani hapa walipokuwa wakiongea kwa nyakati tofauti na waandishi wa habari waliokuwa katika utafiti dhidi ya unyanyapaa na unyanyasaji wa kijinsia, ulioratibiwa na chama cha wandishi wa habari za ukimwi nchini AJAAT kwa msaada toka kwa Watu wa Marekani (USAID), kupitia Futures Group International chini ya mradi wa Health Policy Initiative (HPI).

Amina Kondo, mmoja kati ya watu wanaoishi na virusi vya ukimwi ambaye amejiweka wazi kwa jamii, anasema kuwa unyanyapaa umesababisha baadhi yao kushindwa kuendelea na kufanya shughuli za kiuchumi na kubaki tegemezi huku wengine wakikatisha dozi kukwepa kunyoonyewa vidole na watu wanapokuwa katika vituo vya kuchukulia dawa.

“Mimi nimegundulika kuwa na virusi vya ukimwi tokea mwaka 2004 na kuanza kutumia dawa za ARVs…..lakni wenzangu wengi wameacha kutumia kukwepa kunyooshewa vidole na fya zao hivi sasa ni mbaya……na hata nilipoanza kufanya biashara ya kuuza mihogo watu wakataa kununua kwa vile eti nitawambukiza virusi”, alisema Amina.

Mama huyo mwenye watoto watatu na mbaye amepoteza mume kwa maradhi ya ukimwi. Na mkazi wa Lindi mjini, alisema kuwa kama asingekuwa na ujasiri wa kujitangaza na kuwa wazi kwa jamii ingemuiya vigumu kuendelea na shughuli zake na kutumia dawa hizo.

“Sasa wamezoea na wananunua mihogo kwangu…nadhani upo umuhimu wa watu tuliona virusi hivi kuwa wazi maana hii inaweza kutupunguzia msongo wa mawazo…..na hawa wanowanyooshea vidole wenzao wakapime wajue afya zao maana wengi wao hawajapima”, alisema Amina.

Naye Geoge Simba, mwanachama mwanzilishi wa kikundi cha uzalishji kipato cha watu wanaoishi na virusi vya ukimwi wilayani Kilwa, alisema kuwa licha ya kikundi chao kuwa na wanachama 26 lakini walioamua kuw wazi na kujitangaza kwa jamii ni wane tu huku wengine wkihofu kunyanyapaliwa.

Simba baba wa mtoto mmoja alisema kuwa alipojitangaza kuwa naishi na virusi jamii ya wakazi wa Kijiji cha Ngulukulu anapoishi na kufanya biashra zake walimtenga na kuacha kununua bidhaa zake kwa kuhofia kuambukizwa.


“Mimi na mke wangu tumekuwa tukiishi na virusi vya ukimwi kwa zaidi ya miaka tisa sasa…..lakini mwanzoni tuliyumba sana baada ya jamii inayotuzunguka kutunyanyapaa na kama nisingekuwa jasiri n kusimma imara katika biashara zangu za chips na kuku hali zetu zingezidi kuwa mbaya” lisema Simba.

Mganga mkuu wa mkoa wa Lindi, Dk. Mohamedi Alli, aliwaambia waandisi wa habari kuwa waganga katika hospitali na vituo vyote vya kutolea huduma mkoani umo wamepewa mafunzo yanayowawezesha kuwahudumia wagonjwa wote wkiwemo wale wanaoishi na virusi vya ukimwi ili kuondoa unyanyapaa.

“Hapa katika hospitali ya mkoa tumeweka kituo kimoja ambapo mtu anayeishi na viru vya ukimwi anpta huduma zote…..lakini pia vituo vyote vya kutolea huduma mkoani kwetu waganga wanawahudumia wote hakuna tena utaratubu wa kuwatengea….hii inasaidia kuondoa unyanyapaa …lakini hii ni kwa upande wa afya na ukimwi ni suala mtambuka na wemgine waitmize wajimu wao hili si suala la kihospitali tu” alisema Dk Mohamedi.

Mwisho.

Saturday, July 10, 2010

Mimba za utotoni




Picha: Mwalimu Pili Maximiliani, Mkuu wa Shule ya Kamnyang'anyo sekondari, Wanafunzi wa Shule ya Kamnyang'anyo, Dr Rashidi Shemsanga akiongea na waandishi habari


Uongozi wa Kijiji wazira kushughulikia mimba za utotoni

Na Charles Kayoka

Uongozi wa kijiji cha Magamba, kata ya Kwaluguru, wilayani Handeni wamesema wana mpango wa kutangaza kwa wanakijiji kuwa hawatapokea tena kesi za mimba za wanafunzi kutokana na kukosa ushirikiano na polisi na mahakama wilayani.
Afisa mtendaji wa Kijiji, Hemedi Mbelwa, mtendaji wa kijiji hicho, anasema wameamizia kuitisha kikao cha kamati ya kijiji ili kufikia uamuzi huo na kutoa tangazo kwa wanakijii kuwa kuanzia hapo wanakijiji wasiletea malalamiko tena juu ya watoto wao kupewa mimba.
“hili suala linatuletea ugombanishi na jamii. Tunawakamata wahalifu, lakini polisi na mahakama inawaachia wahalifu ambao wakirudi kijijini wanatuakashifu na tunaonekana sisi wote ni wapumbavu,” alisema.
Aidha mwalimu mmoja wa shule ya msingi aliwahi kukamata mwanamume mtu mzima akifanya mapenzi na msichana wa shule anakofundisha alisema kuwa hatataka tena kujihusisha na suala la mapenzi na mimba za wanafunzi kwa sababu “hakimu wa wilaya aliniuliza maswali ambayo yamenikatisha tamaa.”
Anasema yeye kwa kushirikiana na mgambo mmoja wa kijiji waliweza kumkamata mwanaume huyo na kumfikisha mbele ya sheria kwa matumiani kuwa hatua za kisheria zingechukuliwa, lakini badala yake alionekana kutotoa ushirikiano na hivyo “nikajiona ni mpumbavu kabisa. Kuanzia sasa sitaki tena kujihusisha na masuala haya.”
Hassani Mwachibuzi, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, alipoulizwa na waandishi wa habari kuhusu hatua wanazozichukua kudhibiti mimba za utotoni, alisema kuwa wao hawana majibu kwani hayo yanayotokea ni matokea ya kushindwa kuwa na mikakati ya ziada.
“Huenda nyie mliekwenda huko vijijini na kuongea na wananchi mtupatie mapendekezo ya kutatua haya masuala. Maana sisi tumekuwepo hapa wakati wote na kama mnaona mambo siyo mazuri, basi mjue hapa ndio mwisho wa uwezo wetu,” alisema Mkurugenzi.
Akiongea na waandishi wa habari Kaimu Mganga Mfawidhi wa Wilaya ya Handeni, Dr. Rashid Shemsanga alikiri kuwa tatizo la mimba la utotoni lipo, “na nimewahi kushuhudia watoto wa miaka kumi na tatu wakijifungua hapa. “
Alisema kati ya mwezi Januari 2010 hadi Juni, kwa mujibu wa takwimu za hospitali, jumla ya watoto wa kike 141 wenye umri wa kati ya miaka 15 na 18 walikuja hospitali ya wilaya kujifungua.
Mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Kamnyang’anyo, Bi Pili Maximilian, alikiri kuwepo kwa tatizo la watoto kupata mimba na kuwa mwaka jana jumla ya wanafunzi wanane walipata mimba shuleni kwake.
Wanafunzi waliohojiwa walikiri kuwa wanafunzi wa kike na wa kiume wanafanya mapenzi wakiwa na umri mdogo wakisukumwa na tamaa ya vitu vizuri, umasikini na wazazi walio masikini na wenye watoto wengi kushindwa kutimiza mahitaji ya watoto wao. Na kuwa wasichana wanaoishi gheta katika sekondari za kata ndio wanaoathirika zaidi.
Mwisho.

TANZANIA FAMILY PLANNING/ SRH

www.womensdignity.org

But there are some efforts




Sending messages to community regarding PMTCT. even handwritten posters and messages can do. Taken at Misama dispensary, Handeni district

Traditiona Birth Attendants




Traditional Birth Attendants continue to become the necessary elements in the provision of care for our expectant mothers.
In these photos we see a TBA in her delivery room and examining a pregnant mother, at Misama ward, Handeni district.
district medical officials say the TBA "problem" cannot be eliminate as long as health facilities are few, medical staff are we and enough public education is not given to sensitize community members on the need to use health facilities. In Handeni, for instance, over about thirteen thousand women have been attending clinic for the last year. Only 4800 delivered iin health facilities and 1,800 at TBA houses. But where have the rest, over 7000 gone. There is a possibility that they had delivered at home using "expert" services of their mothers or neighbours who are not trained nor have the requisite skills for managing safe delivery.

vituko vya wakunga 2

SAKATA LA MJAMZITO KUJIFUNGULIA KICHAKANI,MUUGUZI ATOWEKA KITUONI,
Na Anthony Mayunga-Serengeti.

SIKU chache tu baada ya sakata la muuguzi wa Zahanati ya Maji moto
kata ya Busawe wilayani hapa Devotha Thomasi kumfukuza mjamzito na
kujifungulia kichakani,ametoweka kwa muda wa siku nne zahanati
haijafunguliwa.

Kitendo hicho kinachoendelea kuwatesa wakazi wa kata hiyo ambao
wanategemea Zahanati hiyo kwa ajili ya huduma ,licha ya kuwepo
matatizo mengi ya kiutendaji.

Mwananchi Jumapili ilielezwa na Mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho
Johannes Masirori kuwa muuguzi huyo alitoka siku moja tu baada ya tume
iliyoundwa kumchunguza kumaliza mahojiano.

Alisema kuwa toka julai 7 hakuna huduma inayotolewa hapo na hawajui
muuguzi yuko wapi kwa kuwa amekuwa na tabia ya kutoka bila kuagakwa
madai kuwa hawajibiki kwao

“Hapa unadhani nchi haijapata uhuru,maana huduma za afya kama
inavyohubiriwa na viongozi ni tatizo kubwa sana,watu wanafika
kulalamika kwa kukosa huduma,wanalazimika kwenda Iramba zaidi ya
kilometa 30 ,wilaya inajua kilio chetu lakini hawajachukua
hatua,”alisema.

Alibainisha kuwa Zahanati hiyo inategemewa na vijiji vingi ,kufungwa
kwake kunazidi kuwatesa wagonjwa,hasa wanawake wajawazito na watoto
chini ya miaka mitano.

Alisema kuwa kwa kuwa huduma hiyo ni ya msingi sana kwa jamii ,uongozi
wa wilaya unatakiwa kuchukua hatua za makusudi kuhakikisha wanaachana
na tabia ya kulindana bali uwajibikaji.

“Sijui kwa nini wanalinda kwenye maisha ya watu,hilo lililotokea ni
moja tu likajulikana ,yapo mengi makubwa yanajitokeza hajawekwa
wazi,hivyo uwajibikaji utaaidia kunusuru maisha ya watu,”alisema
Mwenyekiti.

Alipotafutwa na Mwananchi jumapili kwa njia ya simu muuguzi huyo
alikiri kutokuwepo kituoni hapo mpaka jumatatu julai 12.

“Niko Mugumu nimekuja kwa matatizo ,nimefunga kwa sababu niko mwenyewe
sasa nitafanyaje mimi,ni kwa sababu ya matatizo yaliyojitokeza
kazini,”alisema.

Kuhusu matatizo yaliyojitokeza kituo kwake alikiri kuwa tume imeundwa
kumchunguza ,lakini anadai yamebebwa na masuala ya siasa kwa kuwa mme
wake anatarajia kugombea udiwani mwaka huu.

“Ni kweli huyo aliyepata matatizo alikuja kwangu nilimwelekeza aende
kituo cha afya Iramba ,kwa kuwa mimba ilikuwa changa na matatizo
,baadae nikasikia mambo kuwa nimemfukuza,”alisema.

Aliongeza kuwa tatizo hilo lilijitokeza kutokana na kuwa mmoja hapo na
kuwa walimkuta akiwa chumba cha chanjo,na kushindwa kuwahudumia na
kuwaelekeza eneo husika,”mimi nasema siasa inaniumiza maana hili
natengenezewa tu,”alidai.

“Kwa kweli mimi ninapata shida sana,niko pekee yangu nimeomba tuwe
wengi,maana naumwa Bp hupanda kila wakati nashindwa kufanya
kazi,lakini wanasema kuwa mimi nawapiga vita wanaoletwa hapa ili niwe
pekee yangu,”alilalama.

Alikiri baada ya sakata hilo tayari ofisi imempanga muuguzi mwingine
kwenda kituoni hapo na ataripoti julai 12 ,kutoka zahanati ya Maburi.
Kuhusu kutumia muda mwingi kufanya kazi zake za kuuza dawa .alidai
kuwa anaifanya baada ya masaa ya kazi ,”duka ninalo lakini nafanya
baada ya masaa ya kazi,”alisema.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Kimulika Galikunga,Mganga mkuu
Dk Salum Manyatta,na katibu wa afya wa wilaya Peter Shilingi
hawakupokea simu zao licha ya kuita kwa muda mrefu ili kutoa ufafanuzi
huo.

Juni 28 mwaka huu muuguzi huyo anadaiwa kumfukuza Esther Thadeus
aliyefika zahanati hapo kwa ajili ya kujifungua,na kulazimika
kujifungulia kichakani ambapo mtoto alifariki muda mfupi kutokana na
kukosa huduma.

Tukio hilo liliibuliwa na Mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho na
kutaarifu uongozi wa wilaya waliolazimika kuunda tume ya uchunguzi
,ambayo haijatoa majibu.

Juhudi za kuwasaka zinaendelea ili kupata majibu ya tume na msimamo wa wilaya .
Mwisho.

Friday, July 9, 2010

Visa vya Wakunga

MJAMZITO ANYIMWA HUDUMA ,AJIFUNGULIA KICHAKANI ,MTOTO AFARIKI BAADA YA
MUDA MFUPI,
Na Anthony Mayunga-Serengeti.
MJAMZITO mmoja mkazi wa kijiji cha Maji moto kata ya Busawe wilayani hapa Esther Thadeus amelazimika kujifungulia kichakani baada ya kunyimwa huduma na muuguzi wa zahanati ya kijijini hapo na kupelekea mtoto kufariki muda mfupi baada ya kujifungua.
Tukio hilo ambalo limewastua watu wengi linadaiwa kutokea juni 28 mwaka huu majira ya saa 7 mchana na linadhihirisha kuwa vifo vingi vya wajawazito na watoto wadogo kutokana na utendaji mbovu wa wauguzi na wakunga.
Akisimulia mkasa huo ambao umelaaniwa na wakazi wa kijiji hicho Mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho Johanes Masirori alisema,tukio hilo lilifanywa siri kubwa na uongozi wa zahanati hiyo na hivyo
hakuweza kujua mapema.
"Nilipata taarifa julai saba nikafuatilia mama aliyepata matatizo na mashuhuda wakaniambia,muuguzi alipoulizwa alionekana kuwa na jeuri ile ile wala hajutii kitendo hicho,nilimtaarifu Mkurugenzi mtendaji juu ya tukio hilo,"alisema.
Mwenyekiti huyo alisema kuwa Mama huyo inadaiwa alifika zahanati hapo akiwa tayari katika hatua ya kujifungua ,lakini muuguzi huyo ambaye yukopekee yake alidai hana nafasi ya kumhudumia.
"Akina mama walimsihi amsaidie mwenzao ,lakini majibu yake yanadaiwa yalikuwa mabaya ,kwamba wasome nao waweze kumsaidia maana yeye ana kazi zake,"alibainisha.
Kutokana na majibu hayo mama huyo alizidiwa na kufikia hatua ya kuhisi haja kubwa ndipo akaenda kichakani ,kabla ya yote akajifungua huku akisaidiwa na wanawake wenzake.
"Hawakuwa na vifaa hivyo walihangaika sana ,maana kondo la nyuma liligoma kutoka,wengine wakalazimika kutafuta wembe madukani ,hata hivyo mara baada ya kutoka kwa mtoto aliaga dunia kutokana na kile kinachodaiwa kuzidiwa kwa kushindwa kutoka mapema,"alisema Mwenyekiti.
Hata hivyo licha ya tatizo hilo kujitokeza muuguzi huyo Devota Thobias hakuweza kumhudumia hali iliyopelekea waende nyumbani kisha kumpeleka kituo cha afya cha Iramba kwa ajili ya matibabu zaidi.
Akizungumzia utendaji wa muuguzi huyo Mwenyekiti alisema kuwa yupo hapo toka mwaka 1984 na ameolewa na aliyewahi kuwa diwani wa kata hiyo ,hivyo anafanya kazi kadri anavyojisikia wala si utaratibu.
"Malalamiko ni mengi juu ya utendaji wake ,anachukua muda mwingi kuuza duka lake la dawa ,wagonjwa mpaka wamfuate kwake hata muda wa kazi,anatuhumiwa kuuza kadi kwa wajawazito ,kuwatoza fedha hata watoto chini ya miaka mitano,tumelalamika hakuna utekelezaji,"alisema.
"Kuna madai hata ya upotevu wa dawa katika zahanati yetu katika mazingira tete,kumbe anahamisha na kuuza dukani kwake,wakuu wake wanaambiwa lakini hakuna hatua yoyote,"alisema.
Alisema Mkurugenzi julai 6 mara baada ya kupata taarifa aliunda tume iliyoundwa na Shadraka Isalo Mwenyekiti,Peter Shilingi katibu wa afya wilaya,Muuguzi mkuu Nyeura,na Winifrida Mwolo mkuu wa kitengo cha mama na mtoto ambao julai 7 walianza kazi yao.
Mkurugenzi mtendaji Kimulika Galikunga alipotafutwa kwa njia ya simu licha ya kuita hakuweza kupokea,na hata alipotumiwa maswali kwa njia ya ujumbe hakuweza kujibu.
Naye muuguzi huyo anayetuhumiwa na sakata hilo alipotafutwa kwa njia ya simu yake ya mkononi hakuweza kupokea licha ya kuita kwa muda mrefu.
Baadhi ya wakazi wa Iseresere kata hiyo ambao wanatembea kilometa zaidi 17 kufika zahanati hapo ,tena wakitumia usafiri wa mikokoteni ya ng'ombe kupeleka wajawaito walidai kutokana na huduma mbaya hujifungulia majumbani .
Walisema kuwa vifo vya wajawazito na watoto wadogo ni vingi kwa kuwa wanalazimika kusafirisha wajawazito kwenda kituo cha afya Iramba ama hospitali ya mkoa Musoma badala ya kwenda hapo kutokana na huduma mbaya.
Juhudi za kumsaka mama aliyepata matatizo na muuguzi huyo zinaendelea ili kujua kwa undani mkasa huo unaokinzana na mikakati ya serikali ya kuhakikisha wanapunguza vifo vya wajawazito na watoto chini ya miaka mitano.

Tuesday, July 6, 2010

There is need for SRH education



The problem of teenage pregnancies has become not only contagious but it is assuming a dangerous dimension as kids of even younger age brackets afe engaging in unsafe sex and getting pregnant. Both communities and the government need to find a common solution to the problem. While parents need to talk to their children about sex values that promote safe sex and delay boys and girls sex debut, the government must engaging the school and also mass media for a kind of education which not only educates youths on SRH maters but als empowers girls so that they can be able to say no when approached by men who have sexual intentions. The school education in general must impart in girls the ambition for high educational and education achievements, and using models for the purpose.

The likeliness of girls like those in the photos who get married or pregnant at their tender and formative ages must be eliminated and completely done away with. This is not a healthy of buil
d this nation. These girls have been found in Hanang, Nkansi and Makete respectively, as young mothers and wives. They are all in their teenage.

Uzazi wa Mpango

Na Ramadhan Libenanga , Morogoro .

Makala .

Familia nyingi nchini zimekuwa na tatizo la watoto wengi kushindwa kupata elimu ya msingi na hata huduma muhimu wakiwa kama watoto ndani ya familia .

Mwandishi wa makala hii fupi amebaini ni hili katika familia nyingi wilayani Mvomero kutokana wazazi wao kutofuata uzazi wa mpango katika familia zao na hivyo kupelekea kuzaa watoto zaidi ya 8.

Bi Hadija Suleiman mkazi wa Embeti (34) wilayani Mvomero mwenye watoto tisa anaelezea sababu kubwa za familia nyingi kuwa na hali duni kimaisha kutokana na kutokuwa na elimu kuhusu masuala ya uzazi wa mpango.

Ambapo anasema kuwa yapo mambo mengi sana yanayosababisha wakina mama wengi kushindwa kutumia njia ya uzazi wa mpango .

Alisema kuwa yapo matatizo ya itikadi za kidini kwa waume zao , ukilitimba ,na ubabe wa waume zao kutokana na ukosefu wa elimu dhidi ya uzazi wa mpango .

Hata hivyo mama huyo anadai kuwa kundi la wanaume wengi bado halina elimu ya kutosha kuhusu mpango mzima wa uzazi wa mpango na hivyo kuwa chanzo kikubwa katika kufanikisha zana nzima ya uzazi wa mpango .

“inapofikia mwanaume akagundua mwanamke umefunga kizazi kwa njia yeyote bila kumshirikisha , basi utapokea kipigo na hata kupoteza ndoa yako “ alisema mama huyo.


Aidha pia mama huyo anadai kuwa pia imani na uzushi uliopo mitaani kuhusu njia hizo za uzazi wa mpango , uwenda ukawa chanzo kikubwa cha wanawake na waume kukataa kujiunga na aina hizo za uzazi wa mpango .

Hata hivyo naye mganga mkuu msaidizi katika hospitali ya Mission ya Bwagala wilayani Mvomero , Bw Mashaka Shemkande .


Bw Shemkunde alikiri wakina mama na wakina baba katika wilaya hiyo bado hawana elimu ya kutosha kuhusu uzazi wa mpango.


Ambapo alisema kuwa kutokana na hali hiyo ndio sababu kubwa inayopelekea kuwepo na vifo vingi vinavyotokana uzazi wa mara kwa mara , ikiwa pamoja na watoto kuzaa kabla ya umri .

Alisema kuwa kwa kipindi cha mwezi januari mpaka mei tayari hospitali hiyo imepokea watoto 1226 waliozaa kabla ya umri wakiwa na miaka kati ya 15 mpaka 16 .


Hata hivyo alisema kuwa hospitali hiyo imejikuta ikipokea wagonjwa wengi kuliko uwezo hasa wenye kesi zinazotokana , ukosefu wa elimu kuhusu uzazi wa mpango .

Mwisho